• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

MAGU YAWAPA MOTISHA WANAFUNZI BORA, SHULE ZILIZONG’ARA 2024

Posted on: April 6th, 2025

HALMASHAURI ya Wilaya ya Magu imegawa tuzo na zawadi mbalimbali zenye thamani ya Sh milioni 15 kwa shule za sekondari zilizofanya vizuri katika matokeo ya mitihani ya kidato cha pili, nne na sita kwa mwaka 2024.

Zawadi hizo ambazo ni vyeti, makombe na fedha tasilimu kwa walimu, zimelenga kuwapongeza na kuwapa motisha ya kuendelea kuwaanda vizuri wanafunzi kwa mitihani inayofuata.


Mbali na walimu wa shule hizo, pia wanafunzi waliofaulu vizuri masomo ya sayansi na hesabu nao pia wamepewa motisha ya fedha taslimu.

Akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika juzi Magu Mjini, Mkuu wa Wilaya Magu, Joshua Nassari ambaye alikuwa ameambatana na Mkurugenzi wa Halmashauri, Mohamed Ramadhani; Katibu Tawala, Jubilate Lawuo na Mbunge wa Magu, Boniventura Kiswaga (CCM), amewapongeza walimu wa shule hizo kwa kuing’arisha wilaya hiyo kwenye sekta ya elimu nchini.

Pia amewataka wanafunzi waliofanya vizuri katika matokeo hayo kuendeleza jitihada zao katika masomo ili kufikia malengo yaliyojiwekea ikiwamo kuendelea na masomo ya elimu ya juu.


Aidha, Mkurugenzi wa wilaya hiyo amesema ufaulu wa kidato cha sita umepanda kwa 0.1% kutoka 99.9% kwa mwaka 2023 mpaka 100% kwa mwaka 2025 ambapo wanafunzi wote walifaulu kwa daraja la I-III hivyo hapakuwepo na daraja la IV wala 0.


Akifafanua zaisi kuhusu ufaulu huo, Afisa Elimu Sekondari Magu, Beatrice Balige amesema ufaulu wa mtihani wa upimaji kitaifa kwa kidato cha pili umepanda kwa 4.6% kutoka 82.1 % ya mwaka 2023 mpaka 86.7% kwa mwaka 2024.

“Ufaulu wa mtihani kitaifa  kidato cha nne umepanda kwa 9.5% kutoka 88% ya mwaka 2023 mpaka 97.5% kwa mwaka 2024.

Mshindi wa kwanza alipata Tshs 1,110,000, mshindi wa pili Tshs 900,000 na mshindi wa tatu tshs 690,000.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • Mchengerwa aagiza maofisa habari kukabidhiwa ofisi

    May 23, 2025
  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • DC NASSARI AONGOZA KIKAO MAANDALIZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU MAGU

    May 21, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa